Thursday, 15 May 2014

SEVILLA BINGWA MPYA KOMBE LA EUROPA 2013/14



Mkosi wa kutokutwaa kombe la Ueropa umeendelea kuiandama timu ya Benefica ya Ureno baada ya jana usiku kukabithiwa kichapo cha matuta manne kwa mawili kutoka kwa vijana wa Uhispania Sevilla.
Baada ya mchezo huo kwisha kwa sare ya mayai 0 -0, hata baada ya dakika 120 matuta yalipigwa na Wareno hao walishindwa kufurukuta na kujikuta wakilia baada ya safari yao yenye matumaini kuzimwa na vijana hao wa Kihispania.
Kwa matokeo hayo ya kusikitisha kwa benefica ambao walipoteza msimu uliopita kwa Chelsea kwa kichapo cha magoli mawili kwa moja….jana walikuwa na hamu ya kunyanyua ndoo hiyo bila mafanikio.
Alikuwa golikipa wa benefica Beto aliyekuwa na kisimati, baada ya kuchomoa penalti mbili  toka kwa mshambuliaji wa Benefica Oscar Cardozo na Rodrigo aliyepiga penalti fyongo, na kuwafanya Sevilla kuibuka na ushindi wa Penalti 4 kwa 2 za Benefica. 
 Ilikuwa penalti ya Kevin Gameiro iliyosababisha mashabiki wa Sevilla kunyanyuka na kupiga mayowe ya shangwe na kuwafanya Benefica wasio na bahati tangu walipotwaa kombe hilo kwa mara ya pili mwaka 1962
Kwa matokeo hayo, ni wazi kuwa Uhispania imeimarika kisoka, hali tukisubiri kuona wababe wa La Liga Atletico Madrid wakikichapa na Real Madrid tarehe 24 mei kunako dimba la Estadio da Luz


No comments: