Wednesday, 14 May 2014

HIKI NDIO KIKOSI CHA GHANA KUELEKEA BRAZILI 2014

 Ghana wanaelekea nchini Brazili wakiwa na kikosi kilichosheheni wachezaji wenye uzoefu mkubwa. Wakiwa na kumbukumbu ya kupoteza uwakilishi muhimu kwenye robo fainali huko bondeni kwa hayati Madiba miaka minne iliyo pita, wanakibarua kikubwa kupambana na wenzio kwenye kundi lao la kifo (G) Linalojumuisha wababe kama, USA, Wareno na Wajerumani.

Hata hivyo Bl
ack stars wanajisifia watu kama, Prince Boateng na mkongwe Michael Essien pamoja na Asamoah Gyan alietumwa hela kwa Waarabu.
Kocha wao mzawa James Kwesi Appiah aliechukua mikoba hiyo mwaka 2012 na kuwa kocha wa kwanza kabisa wa Kiafrica kuchukua majukumu ya kufunza Ghana  kwenye michuano ya kombe la dunia anategemewa kufanya vyema zaidi, haswa kwa kuwa na kikosi hicho kwa muda wa kutosha sasa. 
Kikosi hicho ni kama ifutatavyo
Magolikipa ni:
Fatau Dauda (Orlando Pirates), 
Adam Kwarasey (Stromsgodset),
Stephen Adams (Aduana Stars).
Walinzi: Samuel Inkoom (Platanias), 
Daniel Opare (Standard Liege), 
Harrison Afful (Esperance), 
Jeffrey Schlupp (Leicester), 
John Boye (Rennes), 
Jonathan Mensah (Evian), Jerry Akaminko (Kisehirspor), Rashid Sumalia (Mamelodi Sundowns).
Viungo: Michael Essien (AC Milan), Sulley Muntari (AC Milan), Rabiu Mohammed (Kuban Krasnodar), Kwadwo Asamoah (Juventus), Emmanuel Agyemang-Badu (Udinese), Afriyie Acquah (Parma), Christian Atsu (Vitesse), Albert Adomah (Middlesbrough), Andre Ayew (Marseille), Mubarak Wakaso (Rubin Kazan).
Washambuliaji: Asamoah Gyan (Al Ain), Kevin-Prince Boateng (Schalke 04), Abdul Majeed Waris (Valenciennes), Jordan Ayew (Sochaux), David Accam (Helsingborg).

No comments: