Waandaji wa kombe la copa america Chile, jana wameibuka wababe wa kombe hilo baada ya kuwashinda wapinzani wao wa zamani Argentina kwa matuta kwenye uwanja wa Estadio Nacional mjini Santiago, baada ya mtanange huo kuisha kwa draw ya mayai hata baada ya dakika 120 .
Chile wameshinda kikombe hicho kwa mara ya kwanza kwenye historia yao ya soka mbele ya mashabiki wenye mshawasha wakikombe hicho. hahasa baada ya kukisubiri. Chile wameonesha uwezo mzuri wa kusakata kabumbu haswa baada ya timu kama za Brazili, Argentina na Uruguay kuonesha viwango vya chini.
