Thursday, 5 June 2014

MAXIMO NA YANGA KUNA JIPYA?

Timu ya YANGA inaonesha nia ya dhati ya kumleta kundini  kocha wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania Mbrazili Marcio Maximo. Kocha huyo ambae anasifa ya kandanda safi ya pasi fupi fupi anakaribia kabisa kujiunga na Yanga kwa msimu ujao wa ligi endapo watakubaliana na masharti yake.

RICKIE LAMBERT AINGIA KITANZI NA LIVERPOOL

Rickie Lambert alikamilisha deal ya kuichezea Liverpool wiki iliyopita akiwa mchezaji wa kwanza kujiunga na kikosi hicho cha majogoo wa Anfield kwa Kitita cha paundi milioni 4. 
Akiwa na umri wa miaka 32 Rickie aliyezaliwa  katika jiji la Liverpool na aliyekwenye kikosi cha Uingereza kilichoko njiani kwenda Brazili, anahamia Liverpool akitokea Southampton ambako alikuwa na msimu mzuri huku akicheza mechi 39  na kufunga jumla ya magoli 14 hali akitoa ushirikiano wa magoli 10

DIEGO COSTA KUMALIZANA NA CHELSEA

Mshambuliaji anayeibukia wa Atletico Madrid, Diego Costa amekamilisha vipimo vya afya yake na Chelsea katika uhamisho unaotegemewa kufikia kisasi cha paundi milioni 32. 
Mzaliwa huyo wa Brazili katika jimbo la Lagarto mwenye umri wa miaka  25, ambaye ni sehemu ya timu ya taifa ya Uispania anatakiwa na kocha mkorofi wa maneno Jose  Mourinho ili kuwezesha kikosi cha Chelsea kutwaa mataji msimu ujao. 

Monday, 2 June 2014

TAIFA STARS YAIPA KIBANO ZIMBABWE

Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imeibuka kidedea baada ya kutoka sare na timu ya taifa ya Zimbabwe (The Worriors ) kwenye mchezo uliochezwa Jana mjini Harare. Kwenye mchezo huo sare ya 2 - 2 ilishuhudiwa na mashabiki wapatao 50 000 waliofika  kushuhudia. 

MOYES "NLIKUWA NA MIPANGO YA MUDA MREFU"

Kocha aliyetupiwa virago wa Manchester United David Moyes amesema hana mpango wowote na Kilabu hiyo kwa sasa wala kwa wakati ujao, japo amesema alikuwa na mipango ya muda mrefu ya timu lakini hakupewa

QATAR KUONDOLEWA HAKI YA KUANDAA KOMBE LA DUNIA 2022

Kutokana na kashfa inayokabili mchakato mzima wa kuiteua Qatar kuwa mwandaaji wa kombe la dunia 2022, huenda haki hiyo ikaondolewa endapo itathibitika kuwa maofisa wa ngazi za juu za vyama mbalimbali vya soka walipewa mlungula kupitisha nchi hiyo.