Thursday, 5 June 2014

RICKIE LAMBERT AINGIA KITANZI NA LIVERPOOL

Rickie Lambert alikamilisha deal ya kuichezea Liverpool wiki iliyopita akiwa mchezaji wa kwanza kujiunga na kikosi hicho cha majogoo wa Anfield kwa Kitita cha paundi milioni 4. 
Akiwa na umri wa miaka 32 Rickie aliyezaliwa  katika jiji la Liverpool na aliyekwenye kikosi cha Uingereza kilichoko njiani kwenda Brazili, anahamia Liverpool akitokea Southampton ambako alikuwa na msimu mzuri huku akicheza mechi 39  na kufunga jumla ya magoli 14 hali akitoa ushirikiano wa magoli 10

 ' siamini kuwa ninarudi Anfield, ninaipenda kupindukia klabu hii na ni furaha kurudi kutumikia timu ninayoipenda mno. Nimekuwa na ndoto za kukipiga kwenye timu hii tangu nilipoondoka miaka 17 iliyopita na sijaacha kuipenda liverpool' alisema Lambert

No comments: